Runinga ya Tandao yavumbua jukwaa “GOLIVE AFRIKA”

0
26

Jukwaa mpya la “golive africa” limevumbuliwa ili kusaidia mashabiki wa  televisheni ya Tandao kupata kipindi chochote kwenye televisheni hiyo. Mkurugenzi mkuu wa runinga ya Tandao  Robert Wanyonyi ameeleza kwa ufasaha  jinsi mtu anaweza kupata jukwa hili na jinsi ya kupata kipindi chochote kinachotoka moja kwa moja kwenye televisheni.

Akizungumza wakati alipo kuwa akiwaarifu mashabiki wake, mkurugenzi mkuu wa runinga ya Tandao  Robert Wanyonyi alielezea jinsi jukwaa   mpya iitwayo golive africa inafanya kazi. Jukwaa hili limewekwa ili mashabiki kupata programu zozote katika runinga ya Tandao.

Ameongeza mtu yeyote anaweza kupata vipindi vya televisheni kwenye tovuti ya tandao na kuelezea  kwa ufasaha jinsi mtu anaweza pata jukwaa hili katika simu yake.

Mtu yeyote anaweza kupata vipindi vyote vya Tandao tv kutoka jukwaa la  golive afrika hasa mashabiki waaminifu wa  runinga ya Tandao kutoka Nairobi, Kiambu miongoni mwa wengine ambao wamelalamika kuhusu masuala hiyo ya hali mbaya ya miw3;  Tandao.

Mkurugenzi mkuu wa runinga ya tandao pia ameongeza kuwa mtu yeyote anaweza tazama vipindi vyote kwenye jukwaa hili kutumia hela kidogo.

Alitumia hotuba hiyo pia kuwathamini mashabiki wake waaminifu haswa kutoka mataifa mengine kama Ujerumani urusi Uholanzi na afrika kusini.

By Marion Halil

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here