Afueni kwa wanakandarasi Siaya: Gavana James Orengo atoa amri

0
2

Gavana wa Siaya James Orengo ametupilia mbali agizo la kusitisha malipo ya madeni kwa wanakandarasi waliojitwika majukumu ya kukamilisha miradi mbali mbali na kuagiza malipo hayo yafanywe haraka iwezekanavyo  kulingana na sheria.

Wanakandarasi wa Siaya Orengo aruhusu wanakandarasi walipwe miradi ikaguliwe kabla ya malipo kufanyika gavana Orengo  akihutubia katika bunge la Siaya amesema kuwa serikali yake imekaguwa stakabathi zote muhimu katika hazina ya kaunti hiyo na kufikia hatua hiyo ya  kuwataka wanakandarasi walipwe ujira wao wa baada ya kujitolea katika  kukamilisha miradi mbalimbali ya kaunti hiyo.

Aidha orengo amesema kuwa kuchelewesha kwa malipo hayo kunaathiri  zaidi baadhi ya wanakandarasi na kuwafanya wengine wao kupata  ugumu katika kutekeleza majukumu yao ya binafsi.  

Hivyo basi  orengo ametaka malipo ya wanakandarasi hao kukamilishwa kwa kufuatia ushahidi utakaotibitisha kukamilika kwa miradi iliyotolewa katika kaunti hiyo.

“We have an authorised payment of pending bills but there must be arecosd  when you want to make a payment in a public institution, “ James Orengo says.

 “There must be origination of  a claim there must be a paper trale and when the payment is made there must be  an acknowledgement in writing including  stamps and seals that is the only way that the public or government money must or should be spend.“ James Orengo governor Siaya county.

Licha ya furugu kushuhudiwa  katika kaunti mbalimbali kutokana na hali sawia na hii ya kusitishwa kwa malipo ya wanakandarasi miongoni mwa matukio mengine mengi.

Kaunti hii ya siaya inasemekana kudumisha amani miongoni mwao na zaidi wanaombwa kuendelea kudumisha amani hii ambayo ni adimu katika kaunti mbalimbali.

Wanakandarasi hawa ambao awali malipo yao yalisitishwa sasa wanaenda kupokea maluipo yao kutokana na kauli ya gavana James Orengo. Vile vile ni dhahiri kuwa  malipo haya yatafanyika tu iwapo kutakuwa na shuhuda za kutosha zitakazoonyesha kuwa miradi hiyo ilifanyika na kukamilika kama ilivyoagizwa.

Na Juliet Wekesa

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here