Muhoozi atishia kuliteka jiji la Nairobi huku Uganda ikijitenga na madai hayo

0
13

Muhoozi Kainerugaba, mtoto wa rais wa jamhuri ya Uganda ameondolewa katika nafasi ya kamanda wa vikosi vya nchi kavu vya jeshi la ulinzi la wananchi wa Uganda baada ya kutishia kushambulia nchi ya Kenya kwa maongezi yake katika mtandao wa kijamii wa twita.

Kamanda huyo wa zamani wa UPDF Muhoro, mwanawe rais wa nchi ya Uganda Yoweri Museveni  aliandika kwenye  mtandao wa kijamii wa twita  utata kuhusu demokrasia nchini Kenya, kutoka kwa maoni kwamba rais wa zamani Uhuru Kenyatta alipaswa kugombea muhula wa tatu. Pia aliandika kuwa watavamia nairobi yeye pamoja na jeshi lake’

“Nitalivamia jiji la Nairobi na jeshi langu majumaa mawili yajayo”

Wizara ya mambo ya nje ya Uganda, hata hivyo, ilijitenga na maandishi  haya kwenye mtandao wa twita  ambao ulisababisha ghasia nchini kenya na vita katika mtandaonwa twita baina ya nchi hizi

Wizara hiyo ilisema kuwa hio  serikali ya jamhuri ya Uganda   inapenda kusisitiza ahadi yake ya ujirani mwema, kuishi pamoja kwa amani na ushirikiano

“Serikali ya jamuhuri ya Uganda inapenda kusisitiza ahadi yake ya ujirani mwema amani na ushirikiano”

Wizara ya mambo ya nje inapenda kufafanua kuwa serikali ya jamhuri ya uganda haifanyi sera yake ya mambo ya nje na shughuli nyingine rasmi kupitia mitandao ya kijamii wala haitegemei vyanzo vya mitandao ya kijamii katika kushughulikia serikali nyingine huru,” ilisema wizara hiyo.

Na Marion Wafula

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here