LALA SALAMA ZA RAIS UHURU KENYATTA.

0
7

Rais Uhuru Kenyatta akiwa katika siku za lala salama kabla ya

Kumpisha mrithi wake katika ikulu, mihula yake miwili imekuwa na

Panda-shuka katika uongozi wa taifa, siku chache zilizopita

akiwaongoza wafanyakazi wa ikulu katika hafla ya kustaafu kwake.

Wakenya wamekuwa na hisia mseto kuhusiana na uongozi wa rais

Kenyatta.

Zachariah Barasa aliye mwaniaji wa ubunge Sirisia katika jimbo la

Bungoma, kwa maoni yake asema, serikali ya Jubilee ina mengi ya

Kujivunia, japo eneo la magharibi linaonekana kusahaulika katika

Miradi ya maendeleo liilinganishwa na maeneo mengine.

Rais Kenyatta mara si moja, amesifia salamu zake za heri za machi

Mwalka wa elfu mbili kumi na nane, na aliyekuwa waziri mkuu Raila

Odinga, akisema uhusiano wake mwema na Odinga ndio chanzo cha

Maendeleo na amani katika mhula huu wa pili, akitofautiana na naibu

Wake William Ruto anayeshikilia kuwa ukaribu wa raila serikalini

Ulibadili nia ya serikali, akiongeza kuwa mchakato wa kubadilisha

Katiba bbi ulichukua nafasi ya agenda nne kuu za jubilee.

Geofrey nyage na Patrick Okumu, ambao ni wakaazi wa Nairobi,

Wanakubaliana kuwa Jubilee imefeli wakenya katika vita dhidi ya

Ufisadi.

Viongozi waraiwa kutimiza agenda zao kwa manufaa ya jamii, Ann

Kerubo aliye mkaazi wa Kisii, akiwakumbusha wawaniaji wa vyeo

Mbalimbali kuwa ahadi ni deni, dawa yake ikiwa ni kulipa.

Jacob Macheso

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here