Uchaguzi mkuu unapokaribia nchini, amani yahubiriwa katika pembe

Zote za taifa. Serikali imewahakikishia wakenya usalama hasa wakati

Na baada ya uchaguzi. Macho yote ya serikali, hata hivyo,

Yanaonekana kukodolea tu, agosti tisa, huku baadhi ya wakenya

Wakikumbwa na utovu wa usalama.

John wafula, aliye mmiliki na mwekezaji katika shamba linaloitwa the

Black swan, katika kijiji cha bondeni, lokesheni ya machewa, katika

Eneo bunge la saboti kaunti ya trans nzoia, anakadiria hasara ya

Takriban shilingi milioni mbili, katika shamba lake la ekari arobaini na

Mbili.

Ijumaa ya tarehe ishirini na mbili julai, genge la wahalifu lilivamia

Shamba hilo usiku, likkangamiza na kuiba mali, ikiwemo mizinga mipya

Ya nyuki thelathini na mitano, tanki za maji, nyua, nyumba na mavazi

Wanayotumia wahudumu wa shamba hilo, na vilevile kuchinja na

Kuiba mifugo.

Joseph simiyu, aliye meneja katika shamba hilo, asema maisha yake na

Ya mwajiri wake john yamo hatarini, akiongeza kuwa, wavamizi hao

Walinuia kuyakatisha maisha yake, swala lililombidi kukesha kwenye

Baridi msituni kuyaokoa maisha yake.

Runinga ya tandao ilizuru bondeni katika lokesheni ya machewa,

Mahala pa mkasa, japo kwa ugumu ukizingatiwa uduni wa miundo

Msingi, ikiwemo barabara, ugumu wa kufikia eneo hili ukihitilafu

Pakubwa, upesi wa vitengo vya usalama kuwanusuru wananchi

Patokeapo mikasa kama hii, wakaazi kwa kero, wakikiri kusahaulika na

Viongozi waliowachagua, na kuongeza kuwa serikali imefeli eneo hili

Katika ukuaji wa maendeleo.

Zaidi ya juma sasa tangu uvamizi huo kufanyika, mwekezaji john

Wafula akaaye marekani, na meneja joseph simiyu anayehudumu

Katika shamba hilo, bado wasubiri sheria kuchukua mkondo wake

Dhidi ya wavamizi hao, usemi maarufu kuwa serikali ina mkono

Mrefu, kwao ikisalia tu ndoto ya mchana, wakiendelea kulilia haki,

Kwani haki inayocheleweshwa ni sawa na haki inayonyimwa.

Jamii hii kwenye shamba la the black swan, imebaki na kitendawili cha,

‘je, tutalia hadi lini?’ mwenye kukitegua kitendawili hiki akiwa waziri

Wa usalama wa ndani, dakta fred matiang’i kwa ushirikiano na ocs

Katika kaunti ya trans-nzoia, matumaini ya kufanyiwa haki kutumia

Vitengo vya usalama vya eneo hili yakididimia kila kuchao, kwa kuwa

Hadi sasa hakuna mshukiwa aliyetiwa mbaroni licha ya maafisa wa

Polisi kuaminika kuwafahamu wahusika, kwani wavamizi hao

Waliwatayarisha polisi hao na kuwapa vitisho katika mazungumzo ya

Moja kwa moja kabla ya uvamizi, na polisi hao vilevile wakawarai

Wavamizi kurejesha mbuzi mmoja, kulingana na meneja joseph

Anayeshikilia kuwa matunda ya uchunguzi wa mwendo wa kobe

Unaofanywa na polisi hao huenda usizae matunda.

Jacob Macheso

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here